Kuna haja ya kubadili utawala nchini Urusi - Zelensky
Eric Buyanza
August 1, 2025
Share :

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ametoa wito wa kutaifishwa kwa mali zote za Urusi zilizozuiwa na mataifa ya Magharibi, ili ziweze kuchangia katika kuleta amani na si kuendeleza vita.
Zelensky ametoa wito huo jana Alhamisi wakati akihutubia kwa njia ya mtandao mkutano wa Helsinki, unaoadhimisha miaka 50 tangu kusainiwa makubaliano ya kihistoria kati ya Marekani na Umoja wa Kisovieti yaliyosaidia kumaliza enzi za Vita Baridi.
Rais huyo wa Ukraine ameongeza kuwa kuna haja ya kubadili utawala nchini Urusi, akisema kuwa tofauti na hivyo rais Vladimir Putin ataendelea kuvuruga usalama wa majirani zake.





