pmbet

Miji ya Pokrovsk na Vovchansk yaangukia mikononi mwa Urusi

Eric Buyanza

December 2, 2025
Share :

Makamanda wa kijeshi wa Urusi wamemwambia Rais Putin jana Jumatatu kwamba vikosi vya nchi hiyo vimeiteka miji ya Pokrovsk na Vovchansk nchini Ukraine.

Taarifa hiyo kwa Putin ilisema vikosi hivyo vinaendelea kusonga mbele kwenye maeneo mengine, jambo ambalo rais huyo alijitapa nalo kuwa mafanikio yatakayowezesha kupata ushindi mkubwa zaidi. 

Maafisa wa Ukraine hata hivyo bado hawajathibitisha kwamba maeneo hayo yameangukia mikononi mwa Urusi.
 

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet