pmbet

Saudia kushtakiwa kwa shambulizi la Sept. 9

Sisti Herman

September 3, 2025
Share :

 

Jaji wa nchini Marekani ameruhusu familia za waathirika wa mashambulizi ya Septemba 11 kuendelea na kesi dhidi ya Saudi Arabia, hatua inayofufua mjadala wa muda mrefu kuhusu uwajibikaji.

Familia hizo zinadai kuwa baadhi ya maafisa ndani ya serikali ya Saudi Arabia waliunga mkono magaidi waliohusika na mashambulizi hayo, madai ambayo Saudi Arabia imekanusha kwa nguvu.

Uamuzi huu unafuata kupitishwa kwa sheria ya Justice Against Sponsors of Terrorism Act (JASTA) mwaka 2016, iliyowapa waathirika na familia zao fursa ya kufungua kesi dhidi ya serikali za kigeni zinazoshukiwa kuhusika na ugaidi ndani ya Marekani.

Ingawa mchakato wa kisheria bado unaendelea, uamuzi huu ni hatua kubwa katika kesi inayohusishwa na moja ya siku za majonzi makubwa zaidi katika historia ya Marekani. Kupitia kesi hii, familia za waathirika wanatafuta sio tu fidia, bali pia uwajibikaji.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet