Viongozi wa Rwanda na Kongo kukutana na Trump Alhamis
Eric Buyanza
December 2, 2025
Share :

Rais wa Marekani Donald Trump atakutana na viongozi wa Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo siku ya Alhamisi hii ili kusaini makubaliano ya amani, Ikulu ya White House imesema.
Mkutano huo unatarajiwa kuboresha makubaliano ya amani yaliyosimamiwa na Marekani mwezi Juni na kutiwa saini na mawaziri wa mambo ya nje wa nchi hizo mbili, pamoja na mpango mkakati wa kiuchumi ulioafikiwa mwezi Novemba.





