Wananchi washusha mtambo wa magoli kutoka DR Congo.
Joyce Shedrack
July 31, 2025
Share :
Klabu ya Yanga imemtambulisha rasmi mshambuliaji Andy Bobwa Boyeli (24) kutoka Sekhukhune United ya Afrika Kusini kwa mkopo kwa msimu mmoja wenye kipengele cha kununuliwa mazima.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kabla ya kujiunga na Sekhukhune United alifanikiwa kuwa mfungaji bora wa ligi kuu ya Zambia msimu wa 2022/23 akiwa na Power Dynamos baada ya kufunga magoli 18.





