"Acha nisiseme sana ila heshima yetu imerudi"Ahmed Ally.
Joyce Shedrack
December 20, 2025
Share :
Meneja Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba Ahmed Ally amefunguka kwa mara ya kwanza baada ya klabu hiyo kumtambulisha kocha wake Mkuu siku ya jana Steve Barker kutokea Afrika Kusini.

Ahmed Ally amechapisha ujumbe kwenye ukurasa wake wa Instagram akimsifia kocha huyo wa zamani wa Stellenbosch huku akikiri wazi kuwa heshima yao imerudi.
“Huyu Kocha wetu mpyaaaa aaaah ana hatariii 😀😀 Acha nisiseme sanaaa ila heshima yetu imerudii” Ameandika Ahmed Ally.





