pmbet

Aliyeigiza 'Apocalypto' afariki dunia

Sisti Herman

February 3, 2026
Share :

 

Muigizaji wa kimataifa kutoka nchini Mexico, Gerardo Taracena, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 55.

Ameshiriki katika filamu maarufu duniani zikiwemo Apocalypto, Man on Fire, The Mexican, na Sin Nombre, na aliwafikia watazamaji wa kizazi kipya kupitia mfululizo maarufu wa Netflix wa Narcos: Mexico.

Kifo chake kimethibitishwa mnamo Januari 31, 2026, na Chama cha Kitaifa cha Waigizaji (ANDA), ambacho kilitoa taarifa rasmi kikielezea masikitiko makubwa kufuatia msiba huo. Hakuna maelezo zaidi ya kitabibu au mazingira ya kifo chake yaliyowekwa wazi.

Taracena alitambulika kimataifa kwa uwezo wake mkubwa wa kuigiza na mvuto wa kipekee uwanjani, akijenga taaluma iliyovuka mipaka kati ya sinema za Mexico, Hollywood, na majukwaa makubwa ya kidijitali.

Unakumbuka uhusika wake?
Gerardo Taracena anakumbukwa zaidi na wengi kwa uhusika wake kama "Middle Eye" katika filamu ya Apocalypto, ambapo alionyesha uwezo wa kipekee uliomfanya afahamike kote duniani.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet