Anicet Oura kuivaa Yanga Jumapili.
Joyce Shedrack
May 1, 2026
Share :
Kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Anicet Oura aliyepata majeraha katika mechi ya Fainali ya Muungano Cup dhidi ya Yanga SC amerejea katika uwanja wa mazoezi na yuko tayari kuwavaa Yanga SC, Jumapili.
Mkuu wa Zidara ya Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally amethibitisha urejeo wa nyota huyo pamoja na nyota wengine.
“Oura ambaye alikuwa amepata majeraha na kufanya ashindwe kuendelea na mechi pale Zanzibar anaendelea vizuri pamoja na kina Yussuph Kagoma na Nickson Kibabage wote wako tayari kwa mchezo” alisema Ahmed.





