pmbet

Arsenal kufanya vipimo vya jeraha la Grabiel

Joyce Shedrack

November 17, 2025
Share :

Beki wa Arsenal Gabriel Magalhaes  atafanyiwa tathmini na madaktari wa Arsenal wiki hii wakitaka kujua ukubwa wa jeraha lililomlazimu kujiondoa kwenye kikosi cha timu ya soka Taifa ya Brazil.


Arsenal defender Gabriel Magalhães forced off with injury in Senegal  friendly | Dailysports

Beki huyo aliachwa na Brazil siku ya Jumapili baada ya uchunguzi kuonyesha alikuwa na jeraha la misuli katika goti lake la kulia
Gabriel alipata jeraha Jumamosi wakati Brazil ikishinda 2-0 dhidi ya Senegal kwenye Uwanja wa Emirates.
 

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alichechemea zikiwa zimesalia dakika 30 tu za kucheza na hatasafiri na kikosi cha Brazil kwa mechi yao ya kirafiki dhidi ya Tunisia mjini Lille siku ya Jumanne na badala yake atafanyiwa tathmini na madaktari wa Arsenal wiki hii kabla ya mechi ya London Derby dhidi ya Tottenham, Jumapili hii.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet