Arsenal kutuma ofa nyingine kwa Guimaraes
Sisti Herman
August 3, 2026
Share :

Klabu ya Newcastle United imekataa rasmi ofa ya awali ya Arsenal kwa ajili ya uhamisho wa kiungo Bruno Guimaraes.
Licha ya ripoti za kukataliwa kwa ofa hiyo ya awali, yenye thamani ya takriban pauni milioni 70, klabu hizo mbili zimeacha kutumia madalali na sasa zinafanya mazungumzo ya moja kwa moja kati yao ili kufikia makubaliano.





