Atletico Madrid kumwachia Alvarez kwenda Arsenal kwa masharti.
Joyce Shedrack
July 25, 2026
Share :
Atletico Madrid ipo tayari kuikubali ofa ya Arsenal kwa Julian Alvarez ikiwa dili hilo litahusisha Viktor Gyökeres kuelekea Madrid kama sehemu ya makubaliano.

Alvarez anatajwa kuwa mmoja wa wachezaji wanaowindwa kwa nguvu na Arsenal, ambao wanataka kumleta Emirates msimu huu.
Hata hivyo, ndoto ya Alvarez ni kujiunga na Barcelona. Wakati wa Kombe la Dunia, nyota huyo wa zamani wa Manchester City alifichua kuwa tayari amezungumza na Atletico kuhusu kutimiza ndoto yake ya kucheza Camp Nou.





