Baba mzazi wa Lamine Yamal ashambuliwa kwa visu Hispania
Sisti Herman
August 15, 2024
Share :
Baba mzazi wa kiungo mshambuliaji wa klabu ya Barcelona na timu ya Taifa ya Hispania Lamine Yamal, Bwana Mounir Nasraoui jana usiku ameripotiwa kwa kuchomwa visu kwenye maegesho ya magari Mataro jiji Barcelona nchini Hispania.
Kwa mujibu wa Mundo Yamal Mounir alipelekwa hospitali kuu ya Catalan akiwa kwenye uangalizi maalumu huku polisi tayari wameanza kuchunguza kisa hiki.
Hadi sasa polisi wafanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne wa tukio hilo.