Bajaber aongozana na Simba safari ya kwenda Zenji.
Joyce Shedrack
April 22, 2026
Share :
Kiungo mshambuliaji wa Simba SC Mohamed Bajaber ameongozana na kikosi hicho katika safari ya kwenda Zanzibar kwa ajili ya kushiriki Mashindano ya Muungano.

Bajaber raia wa Kenya aliyetolewa katika mfumo wa usajili kimataifa ameungana na kikosi hicho kilichokwenda leo visiwani humo kwa ajili ya mashindano hayo.
Mara ya mwisho kiungo huyo kuonekana uwanjani alikuwa akiitumikia Kenya katika Mashindano ya FIFA Series.





