Bendera ya Tanzania ipo mikono salama Nchini Saudi Arabia.
Joyce Shedrack
April 25, 2026
Share :
Nyota wa Timu ya Taifa ya Tanzania Clara Luvanga kwa mara ya pili mfululizo ametwaa ubingwa wa ligi ya wanawake Saudi Arabia akiwa na Al Nassr huku akifanikiwa kushinda tuzo ya mfungaji bora wa ligi hiyo.
Clara Luvanga ametwaa tuzo hiyo ya mfungaji bora wa ligi akifunga mabao 24 kwenye michezo 14 mabao 5 zaidi ya yale aliyoyafunga msimu uliopita.





