Bruno avunja rekodi ya David Beckham EPL
Sisti Herman
March 16, 2026
Share :

Kiungo mpisho wa Ureno na klabu ya Manchester United, Bruno Fernandes sasa ameweka rekodi ya kutoa pasi nyingi zaidi za mabao katika msimu mmoja wa Ligi Kuu kwa mchezaji wa United na anakuwa mchezaji wa tatu pekee katika historia ya klabu kufikisha mabao 100 na asisti 100.
Wakati huo huo, Michael Carrick pia anaingia kwenye vitabu vya historia kama meneja wa kwanza kushinda mechi zake sita za kwanza za Ligi Kuu ya Uingereza akiwa na klabu hiyo.





