Bubista apewa timu RS Berkane
Sisti Herman
August 4, 2026
Share :

Pedro Leitão Brito, anayefahamika zaidi kama Bubista, ameteuliwa rasmi kuwa kocha mkuu mpya wa klabu kubwa ya Morocco, RS Berkane, kwa mkataba wa miaka miwili utakaodumu hadi mwaka 2028.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 56 aliamua kuondoka katika wadhifa wake baada ya kipindi cha kihistoria cha miaka sita na timu ya taifa ya Cape Verde ili kukabiliana na changamoto hii mpya katika soka la ngazi ya klabu.





