Cambodia yaamuru waafrika wote kuondoka nchini humo
Eric Buyanza
May 29, 2026
Share :

Serikali ya Cambodia imetoa notisi ikiagiza raia wote wa Afrika, wakiwemo raia wa Kenya, Ghana, Cameroon na Uganda, kuondoka nchini humo ifikapo Mei 31, 2026, au watakamatwa na kushtakiwa chini ya sheria za uhamiaji.
Notisi hiyo inaongeza kuwa raia yeyote wa kigeni atakayepatikana nchini humo kuanzia Juni 1 atakamatwa katika uwanja wa ndege au sehemu yoyote atakayopatikana.
Kwa mujibu wa agizo hilo, watakaobainika kukiuka masharti hayo wanakabiliwa na kifungo cha miaka miwili jela na faini ya dola 800 kabla ya kuruhusiwa kuondoka nchini humo.
Tangazo hilo limeibua wasiwasi miongoni mwa mashirika ya kutetea haki za kibinadamu wakitaja kuwa waafrika walioko Cambodia walijipata huko baada ya kuhadaiwa kuwa kuna kazi za mishahara ya kuridhisha.
Idadi kubwa ya wakenya walioko Kusini mwa Asia kama vile Cambodia, Myanmar na Laos wamekuwa wakitaka serikali ya Kenya kuwafadhili ili kuwarejesha nyumbani wakilalamikia kuwa hawamudu gharama za usafiri.
BBC





