pmbet

China wana furaha kufunguliwa kwa mlango wa Hormuz - Trump

Eric Buyanza

April 18, 2026
Share :

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema kuwa Rais wa China, Xi Jinping, “ana furaha sana” kuhusu hali ya kufunguliwa kwa mlango bahari wa Hormuz, huku akieleza matarajio makubwa ya mkutano wao ujao nchini China.

 

Kupitia mtandao wake wa Truth Social, Trump alisema kuwa Xi ameridhishwa na hatua ya kufunguliwa kwa njia hiyo muhimu ya usafirishaji wa mafuta duniani.
 

Aliongeza kuwa mkutano wao ujao nchini China utakuwa wa kipekee na huenda ukawa wa kihistoria, akisisitiza kuwa mambo mengi yanatarajiwa kufikiwa kupitia mazungumzo hayo.
 

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Xi Jinping anatarajiwa kukutana na Trump katikati ya mwezi ujao, ambapo ajenda kuu itajumuisha masuala ya amani katika eneo la Mashariki ya Kati, hasa katika muktadha wa mvutano unaoendelea kuhusisha Iran na washirika wake.
 

China amekuwa mdau mkubwa wa mafuta kupitia njia hiyo ya muhimu ya kupitisha mafuta duniani - Hormuz.
 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet