Clara atupia Hat-trick Saudia
Sisti Herman
February 2, 2025
Share :
Nyota wa timu ya Taifa ya Tanzania Clara Luvanga ameisaidia timu yake ya Al Nassr FC kupata ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Eastern Flames kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya wanawake Saudi Arabia.
Katika mchezo huo Luvanga amefunga mabao matatu (Hat trick) na kufikisha jumla ya mabao 13 kwenye mbio za kuwania ufungaji bora.