Davies afikiria kustaafu kucheza soka kisa majeraha
Sisti Herman
March 13, 2026
Share :

Ulimwengu wa soka umeshtushwa na ripoti zinazodai kuwa nyota wa kimataifa wa Canada, Alphonso Davies, anafikiria kuachana na soka la ushindan.
Beki huyo mwenye umri wa miaka 25 amepata jeraha jingine hivi karibuni katika mchezo dhidi ya Atalanta, ikiwa ni mfululizo wa matatizo ya majeraha yanayomwandama.
Inasemekana kuwa maumivu ya mwili na shinikizo la kisaikolojia linalotokana na majeraha ya mara kwa mara yamemfanya Davies kutafakari kwa kina kuhusu mustakabali wake, licha ya kuwa bado yuko katika umri wa kiwango cha juu.





