Diallo na Baleba hawatacheza leo dhidi ya Ipswich
Sisti Herman
August 29, 2026
Share :

Kocha wa Manchester United Michael Carrick amethibitisha kuwa wachezaji Amad Diallo na Carlos Baleba watakosa mchezo wa leo dhidi ya Ipswich kutokana na majeraha.
Baleba atakuwa nje kwa 'wiki kadhaa kutokana na tatizo dogo la kifundo cha mguu'. Carrick anatarajia kuwa Amad atarejea kabla ya mapumziko ya mechi za kimataifa.





