Diamond atajwa kuwa mtu maarufu zaidi Tanzania.
Joyce Shedrack
February 6, 2026
Share :
Msanii maarufu wa muziki kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, ametajwa na majarida mbalimbali ya kimataifa kuwa miongoni mwa watu mashuhuri zaidi kutoka nchini Tanzania.

Umaarufu wake umetokana na mafanikio makubwa katika muziki wa Bongo Fleva na ushawishi wake mkubwa barani Afrika, pamoja na tuzo na ushirikiano wa kimataifa uliomuweka kwenye ramani ya dunia.





