pmbet

Diamond Platnumz atangaza Lavalava kujitoa WCB Wasafi.

Joyce Shedrack

May 21, 2025
Share :

Staa wa muziki wa Bongofleva na Mmiliki wa lebo ya WCB Wasafi, Diamond Platnumz amethibitisha kumruhusu Msanii wake Lavalava kwenda kujitegemea mwenyewe bila kumlipa gharama zozote.

Lava Lava Ft Diamond Platnumz - Kibango (Official Music Video) #2024
Diamond amesema hayo siku ya leo wakati akizungumza na waandishi wa habari Hyatt Regency Hotel  alipokuwa akitangaza kuongeza mkataba mpya wa kuendelea kuitangaza moja ya kampuni ya vinywaji Tanzania.

 

“Lavalava ni moja ya wadogo zangu ambao nawapenda sana hakunifata kuniomba kuondoka  mimi nilimpigia Kim nikamwambia mwambie Lavalava kama kutoka aje nitampa free release”amesema Diamond.

 

Aidha,Msanii huyo amesema ikitokea msanii anayetaka kutoka WCB ametozwa fedha basi ni kwa sababi amemkosea adabu na si vinginevyo.

 

“Ukiona mtu nimemtoza hela ujue kanikosea adabu” Diamond Platnumz.

 

 

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet