DR Congo yathibitisha Ebola haitawazuia kushiriki Kombe la Dunia.
Joyce Shedrack
May 28, 2026
Share :
Shirikisho la Mpira wa Miguu DR Congo limethibitisha kuwa timu yao ya taifa itashiriki Kombe la Dunia baada ya kukidhi masharti ya Marekani ya kupambana na ugonjwa wa Ebola na ni baada ya FIFA kuwathibitishia timu hiyo na benchi la ufundi wataweza kusafiri kushiriki mashindano hayo makubwa ya soka duniani.
Awali kulikuwa na mashaka kuhusu ushiriki wa Kongo kwenye michuano hiyo kutokana na kuzuka ugonjwa wa Ebola mashariki mwa taifa hilo hali iliyopelekea kuchukua uamuzi wa kuhamisha kambi kutoka mji mkuu Kinshasa kwenda nje ya nchi ili kutimiza sharti la Marekani la kutaka wote wanaoomba viza kukaa karantini kwa muda wa 21 kabla ya kuingia nchini humo.
Marekani, Canada na Mexico ndio wenyeji wa Kombe la Dunia mwaka huu kuanzia Juni 11 hadi Julai 19.





