pmbet

Dunia iko kwenye tishio la mlipuko mpya wa Ukimwi - UNAIDS

Eric Buyanza

July 29, 2026
Share :

Dunia iko katika hatari ya mlipuko mwingine wa Ukimwi baada ya ufadhili wa kimataifa kupungua kwa karibu theluthi moja mwaka jana, shirika la Umoja wa Mataifa linalopambana na Ukimwi limesema siku ya jana Jumatatu.
 

Kabla ya Rais Donald Trump kurudi Ikulu ya White House Januari 2025, Marekani ilifadhili 75% ya juhudi za kimataifa za kukabiliana na UKIMWI. Mwezi huo huo, aliagiza kusitishwa kwa muda kwa ufadhili wote unaohusiana na vita dhidi ya Ukimwi kabla ya kurejesha programu za kuokoa maisha siku chache baadaye, ingawa juhudi nyingi za kuzuia zilipunguzwa.
 

Katika ripoti yake ya kurasa 60 iliyozinduliwa huko Brazil kuelekea kuanza kwa Kongamano la Kimataifa la Ukimwi, Umoja wa Mataifa unasema jamii ya kimataifa imeingia katika enzi za siasa na ubanaji wa fedha mambo yanayotishia kuharibu mazuri yote yaliyopatikana kwa miongo kadhaa katika vita dhidi ya virusi hivyo.

 

"Jumuiya ya kimataifa inakabiliwa na kipindi cha msukosuko mkubwa wa kisiasa na kifedha unaotishia miongo kadhaa ya juhudi zilizopatikana kwa bidii katika mapambano dhidi ya UKIMWI," UNAIDS ilisema katika ripoti yake ya kurasa 60 iliyotolewa wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kimataifa wa Ukimwi nchini Brazil.

 

"Bila kujitolea na kuchukua hatua mpya, dunia iko katika hatari ya mlipuko mwingine wa UKIMWI."

 

Ufadhili umepungua kwa asilimia 18 hadi dola bilioni 7.3 mwaka 2025, kiwango chake cha chini kabisa katika karibu miaka 20, ripoti hiyo ilisema. Hali hii inatishia kufuta maendeleo ambayo yamepunguza maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI na vifo vinavyohusiana na UKIMWI hadi viwango vyao vya chini kabisa katika zaidi ya miaka 30.
 

REUTERS

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet