Emam Ashour kwenye rada za Celtic
Sisti Herman
July 12, 2026
Share :

Klabu ya Celtic ya nchini Uskochi wanafuatilia kwa umakini uwezekano wa kumsajili kiungo mahiri wa Al Ahly, Emam Ashour.
Kufuatia kiwango chake bora katika Kombe la Dunia la 2026, ambapo alifunga mabao muhimu dhidi ya Ubelgiji na Australia, klabu hiyo ya Scotland imeanza mazungumzo ya awali na timu ya mchezaji huyo.
Huku Emam Ashour akiwa na mkataba hadi mwaka 2028, Celtic wanajiandaa kujadili ada ya uhamisho, ambayo inaripotiwa kuanzia pauni milioni 4, ingawa matarajio ya Al Ahly huenda yakawa ya juu zaidi.
Hatua ya Celtic kuulizia masharti ya kifedha kwa ajili ya usajili wa kudumu inaashiria nia yao ya kumsajili kiungo huyo mwenye kipaji kikubwa.





