Eto'o ahusishwa kutemwa kwa Aboubakar Cameroon
Sisti Herman
December 11, 2025
Share :

Mzozo mpya umeibuka katika soka la Cameroon huku Samuel Eto’o, rais wa Shirikisho la Soka la Cameroon (FECAFOOT), akishutumiwa kwa kupanga mpango wa kumtenga mshambuliaji nyota Vincent Aboubakar kutoka kikosi cha Indomitable Lions kwa ajili ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) la 2025.
Kulingana na ripoti ya The Sun, Eto’o inadaiwa aliwashawishi benchi la ufundi la timu ya taifa kumwacha mshambuliaji huyo wa Beşiktaş katika juhudi za kulinda rekodi yake ya muda mrefu ya kufunga mabao katika AFCON.
Chapisho hilo linadai kwamba gwiji huyo wa zamani wa Barcelona na Inter Milan hakumtaka Aboubakar, ambaye amekuwa katika kiwango kizuri kwa Cameroon katika mashindano ya hivi karibuni, akikaribia kuzidi idadi yake ya magoli.
Aboubakar, nahodha wa timu ya taifa na mmoja wa washambuliaji wenye uzoefu mkubwa wa Cameroon, alitarajiwa sana kuongoza safu hiyo katika mashindano hayo nchini Morocco.
Kiwangi cha Aboubakar alichokionyesha katika michuano ya 2021—ambapo alifunga mara nane—kilichochea majadiliano kuhusu uwezo wake wa kuipiku rekodi hiyo.





