pmbet

FBI kutoa milioni 500 kwa atakayempata jasusi huyu

Eric Buyanza

May 15, 2026
Share :

Kitengo cha kijasusi cha Marekani cha FBI kimetangaza zawadi ya dola 200,000 kwa yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kumkamata Monica Witt, afisa wa zamani wa ujasusi wa anga na upelelezi wa kijeshi.
 

Katika taarifa iliyotolewa Alhamisi Mei 14, FBI ilieleza kuwa Witt aliwahi kuhudumu katika jeshi la anga la Marekani kati ya mwaka 1997 na 2008, na baadaye kufanya kazi kama mwanakandarasi wa serikali ya Marekani hadi mwaka 2010. Ilisema majukumu yake yalimpa upatikanaji wa taarifa za siri na za juu kabisa kuhusu ujasusi wa kigeni na upelelezi wa kijeshi, ikiwemo utambulisho wa maafisa wa siri wa taasisi za ujasusi za Marekani.

 

Kwa mujibu wa FBI, Witt alikimbilia Iran mwaka 2013. Inadaiwa kuwa baadaye alitoa taarifa kwa serikali ya Iran zilizoathiri usalama wa taarifa za siri za ulinzi wa taifa la Marekani na programu zake za kijeshi.

 

Aidha, anatuhumiwa kufichua taarifa zilizohatarisha maisha ya wanajeshi wa Marekani walioko nje ya nchi pamoja na familia zao, na pia kuwasaidia Wairani kuwatafuta maafisa wa zamani wa serikali ya Marekani ili washambuliwe.

 

FBI imesema kuwa licha ya shtaka dhidi yake, bado hayupo mikononi mwa sheria.

Mwisho wa taarifa hiyo, FBI imetangaza zawadi hiyo ya dola 200,000 na kuomba ushirikiano wa umma katika kumsaidia kumtafuta na kumkamata afisa huyo wa zamani wa ujasusi.

 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet