Ferguson alimuomba Mourinho aende United, Mourinho akakataa
Sisti Herman
August 10, 2026
Share :


Kocha wa Real Madrid José Mourinho amefichua alikuwa mmoja wa makocha waliopendekezwa kumrithi Sir Alex Ferguson huko Manchester United mnamo mwaka wa 2013 kwa ombi maalum la kocha huyo aliyeachana na ukocha mwaka huo.
Hata hivyo, alibadili uamuzi wake kwa hisia kali na kumpigia simu Ferguson huku akitokwa na machozi ili kujiondoa kwenye makubaliano hayo, kwa kuwa tayari alikuwa ameahidi kurejea Chelsea.





