FIFA yakataa rufaa ya Nigeria kuhusu DRC kucheza Play Off
Sisti Herman
February 16, 2026
Share :

Shirikisho la soka duniani (FIFA) limeamua kuwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo haikuvunja kanuni zozote wakati wa mchezo wa mchujo wa kufuzu Kombe la Dunia 2026 dhidi ya Super Eagles.
Awali Nigeria ilikata rufaa kuhusu suala hilo ikinga DRC kufuzu hatua inayofuata ya mtoano kuwania kucheza Kombe la Dunia 2026.
Uamuzi huu unathibitisha kuondolewa kwa Nigeria na kuimarisha nafasi ya DR Congo kuelekea mechi za mchujo za mabara (intercontinental playoffs).





