Gen Z wana kiwango cha chini cha akili (IQ) kuliko kawaida
Sisti Herman
February 15, 2026
Share :

Kuna tafiti zimeanza kuonyesha kuwa baadhi ya vijana wa Gen Z(Gen Z ni watoto waliozaliwa takribani kati ya mwaka 1997 hadi 2012.) wanapata alama za chini kwenye vipimo vya IQ na masomo ya kawaida ukilinganisha na vizazi vilivyopita.
Wataalamu wanataja sababu kama:
– muda mwingi kwenye simu na mitandao
– kupungua kwa muda wa kusoma kwa kina
– utegemezi mkubwa wa teknolojia kwa kila kitu hasaa AI.
Lakini pia kuna upande mwingine wa mjadala. Dunia ya leo ni tofauti sana — Gen Z wamekua kwenye teknolojia, wana ujuzi wa kidigitali, ubunifu na kasi ya kujifunza vitu vipya ambayo vipimo vya zamani huenda havipimi vizuri.





