Guardiola aweka historia baada ya kuinyoa Arsenal
Eric Buyanza
April 20, 2026
Share :

Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola, Jumapili ameweka historia baada ya timu yake kuishinda Arsenal 2-1 kwenye Ligi Kuu ya Uingereza.
Kwa mujibu wa OptaJoe, matokeo ya mchezo huo yanamaanisha kuwa Guardiola sasa ameshinda mechi zake zote nne za Ligi Kuu dhidi ya vinara hao wa Ligi.
Kikosi cha Guardiola kitamenyana na Burnley Jumatano katika mechi yao ijayo ya Ligi Kuu.
Sasa wako pointi tatu nyuma ya kikosi cha Mikel Arteta kwenye msimamo wa ligi wakiwa na mchezo mkononi.





