Gundu la Fadlu kushinda mechi za dabi limehamia Morocco
Sisti Herman
May 11, 2026
Share :

Aliyekuwa kocha mkuu wa klabu ya Simba Fadlu Davids ameendeleza rekodi mbaya ya kutoshinda mechi za dabi kwenye nchi 2 tofauti, Tanzania na Morocco akiwa na Simba SC pamoja na Raja AC.
Kwenye mechi 4 za dabi ya Kariakoo dhidi ya Yanga akiwa na Simba, Fadlu amepoteza mechi zote 4 huku kwenye mechi 3 za dabi ya Morocco dhidi ya Wydad AC akiwa na Raja AC amepoteza mechi 2 na kupata sare 1 tu.






