Gustave Kubwayo na Kanali Nzenze wapigwa vikwazo na Marekani
Eric Buyanza
June 3, 2026
Share :

Marekani imewawekea vikwazo makamanda wawili wa makundi yenye silaha wanaotuhumiwa kuchochea ghasia na ukosefu wa utulivu mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumanne, Ofisi ya Idara ya Hazina ya Marekani ya Udhibiti wa Mali za Kigeni (OFAC) iilimwekea vikwazo Gustave Kubwayo, iliyemtambua kama kamanda wa kitengo cha kijasusi na operesheni maalum cha Forces for the Liberation of Rwanda (FDLR).
Wakati huo huo, John Imani Nzenze, aliyesemekana kuwa kamanda na mkuu wa upelelezi wa kundi la waasi la M23 pia aliwekewa vikwazo.
"FDLR na M23 wameteka maeneo kwa kutumia nguvu na kuua raia mashariki mwa DRC," taarifa kutoka Idara hiyo ilisema.
Iliongeza kuwa: "Kutokana na hatua ya leo, mali na maslahi yote katika mali ya watu waliotambuliwa au waliozuiwa walioelezwa hapo juu ambazo ziko Marekani au katika milki au udhibiti wa watu wa Marekani zimezuiwa."





