Hadithi fupi ya dogo aliyemtabiria makubwa Guardiola
Eric Buyanza
May 29, 2026
Share :
Sikia hadithi hii ya kufurahisha. ❤️
▪️ Nyuma kidogo mwaka 2016, shabiki wa Manchester City mwenye umri wa miaka 7 aitwaye Braydon alijikuta amepanda teksi moja na Pep Guardiola ambaye alikuwa akielekea kwenye kibarua chake cha Man U kwa mara ya kwanza.
▪️ Braydon alimtazama Pep na kumwambia: “Utashinda kila kitu ukiwa na City.”
▪️ Pep alijibu kwa urahisi: "Tutajaribu."
▪️ Miaka 10 baadaye, Braydon sasa ana umri wa miaka 17 na anafanya kazi kama mwandishi wa habari.
▪️ Wikiendi iliyoisha wakati wa kuagwa kwa Guardiola, Braydon alifanikiwa kupiga picha moja ya mwisho na kocha huyo ambaye aliishia kushinda kila kitu Manchester City kama alivyoahidiwa na dogo mwaka 2016.






