Hali ipo shwari sasa kwa Lookman na Osimhen
Sisti Herman
January 8, 2026
Share :

Wachezaji wa timu ya Taifa ya Nigeria Ademola Lookman na Victor Osimhen wamemaliza tofauti zao baada ya sintofahamu iliyokuwepo kati yao wakati wa mchezo wa mtoano dhidi ya timu ya taifa ya Msumbiji walipozozana hadharani.
Kwa Pamoja wachezaji hao wamedhamiria jukumu kamili la Nigeria kushinda taji la AFCON 2025 kuelekea mchezo wa robo fainali dhidi ya timu ya Taifa ya Algeria





