Hali ya uwanja yatia shaka Uingereza mchezo wao wa kirafiki.
Joyce Shedrack
June 6, 2026
Share :
Maandalizi ya Kombe la Dunia ya Uingereza yamekumbwa na wasiwasi juu ya uwanja ambao unaweza kuwa mbaya kwa mechi ya kirafiki
Jumamosi dhidi ya New Zealand na hali ya hewa ya mvua isiyotarajiwa huko Florida, ingawa kocha Thomas Tuchel amesema atashikilia mipango yake.

Uingereza wanatumia mechi hiyo mjini Tampa, ikiwa ni mechi ya kwanza kati ya mbili katika kujiandaa kabla ya mechi yao ya kwanza ya Kundi L dhidi ya Croatia mnamo Juni 17 mjini Dallas, hii ikiwa ni kuwasaidia wachezaji kuzoea joto na unyevunyevu.
Picha za uwanja wa mechi ya kirafiki ya Jumamosi zimezua wasiwasi kuhusu ubora wa sehemu ya kuchezea na uwezekano wa majeraha.





