Harry Kane anaamini atashinda Ballon d'Or kama Nchi yake ikibeba Kombe la Dunia.
Joyce Shedrack
June 4, 2026
Share :
Mshambuliaji wa Bayern Munich na Timu ya Taifa ya Uingereza Harry Kane anaamini kama Taifa lake litafanikiwa kushinda Kombe la Dunia basi atafanikiwa kutwaa tuzo ya Ballon d'Or.
“Bila shaka mimi ni miongoni mwa vipenzi vya kushinda Ballon d’Or. Ikiwa Uingereza itashinda Kombe la Dunia, basi ni rahisi kuona mchezaji wa Kiingereza akishinda tuzo hiyo.”
“Ukiangalia wanaopewa nafasi kubwa ya kushinda: kuna mimi, Olise, na wachezaji waliocheza fainali ya Ligi ya Mabingwa...”
“Niliona kuwa hafla ya utoaji wa tuzo itafanyika London, na huenda hiyo ikawa ishara nzuri kwangu. Kushinda tuzo hiyo katika mji wangu wa kuzaliwa kungefanya jambo hilo kuwa la kipekee zaidi.”