Hasheem Thabeet apitishwa kugombea Urais TBF
Sisti Herman
February 27, 2026
Share :

Nyota wa zamani wa Ligi ya Mpira wa Kikapu Marekani (NBA), Hasheem Thabeet amepitishwa kugombea Urais wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF) baada ya Usaili uliofanyika Februari 27 ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Dodoma Jijini Dodoma.
Taarifa hiyo imetolewa na serikali kupitia Baraza la Michezo la Taifa (BMT) iliyo chini ya Wizara yenye dhamana ya Michezo.





