pmbet

Hatuna uhaba wa silaha, tuna akiba kubwa - Trump

Eric Buyanza

August 7, 2026
Share :

Rais Donald Trump amekanusha ripoti kwamba Marekani inakabiliwa na uhaba wa zana za kivita na kuahidi kupitia ujumbe wa mitandao ya kijamii kutaka "vifungo virefu gerezani" kwa wale wanaoshukiwa kuvujisha taarifa.
 

"Marekani ina akiba kubwa ya 'zana za kivita,' hasa za aina fulani," Trump aliandika kwenye mtandao siku ya Alhamisi asubuhi. "Aidha, kiasi kikubwa kinatengenezwa na kusafirishwa kuja Marekani kadiri ya mahitaji."

 

Trump na Pentagon wanakabiliwa na maswali yanayoongezeka kuhusu hali ya akiba ya silaha za jeshi, huku vita hivyo vikiwa sasa katika mwezi wa sita na makubaliano ya amani yakionekana kutofikiwa.

 

Iran ilijibu ripoti kuhusu kupungua kwa akiba ya Marekani kwa kusema kuwa silaha zake zinazotengenezwa nchini humo zinaiwezesha kukabiliana na "tishio lolote".

 

"Kila siku, dalili za kupungua kwa uwezo wa adui zinazidi kudhihirika," Waziri wa Ulinzi Majid Ibn-e-Reza aliandika kwenye mtandao wa X. "Lakini Majeshi yetu - yakisaidiwa na sekta ya ulinzi ya taifa - yana vifaa vya kutosha kukabiliana na tishio lolote."

 

Aliongeza kuwa "wale wanaotaka kununua usalama na ubora wa kijeshi kupitia mifumo iliyoagizwa kutoka nje hivi karibuni watagundua kuwa teknolojia ya ndani ya Iran ni bora zaidi kuliko mfumo wowote katika eneo hili".
 

Baada ya Marekani kutumia kiasi kikubwa cha silaha ambazo ni ngumu kutengenezwa wakati wa operesheni ya kivita inayojulikana kama 'Operation Epic Fury' na mashambulizi ya kulipizana kisasi yaliyofuata, utawala wa Trump umejaribu kuwahakikishia Wamarekani kuwa akiba ya makombora ya nchi hiyo bado ni imara.
 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet