Hii ndiyo sababu ya Al Qaeda kuwa kimya juu ya vita vya Iran
Eric Buyanza
April 23, 2026
Share :

Al-Qaeda imekuwa kimya sana kuhusu vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vilivyoanza Februari 28. Hili si jambo la kawaida, kwani al-Qaeda na wafuasi wake kwa kawaida wamekuwa wakijihusisha na matukio makubwa ya Mashariki ya Kati.
Hasa wakati ambapo migogoro kama hiyo inajadiliwa ndani ya makundi yenye msimamo mkali.
Mwaka huu, kauli moja tu ilitoka kwa uongozi mkuu wa Al-Qaeda, Februari 4, wakati ambapo Marekani ilikuwa ikiongeza uwepo wake wa kijeshi Mashariki ya Kati, kufuatia mvutano na Iran.
Taarifa yake ilitoa wito wa kufanyika mashambulizi dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani na Israel, na mashirika mengi yenye msimamo mkali yaliiona taarifa hiyo kama ya kuuunga mkono Iran kwa njia isiyo ya moja kwa moja.
Lakini hakujawa na kauli nyingine zaidi ya hiyo. Kundi hilo kwa sasa liko katika hali ngumu. Kiongozi wake, Saif al-Adl, na washirika wake wa karibu wanaaminika kuishi Iran kwa mujibu wa FBI.
Baada ya mashambulizi ya 9/11, viongozi wengi muhimu wa Al-Qaeda na familia zao walikimbia Afghanistan na Pakistani na kwenda Iran.
Kwa upande mwingine, al-Qaeda huenda inakwepa kuikera Iran, ndiyo maana haijajiunga waziwazi na makundi yenye msimamo mkali ambayo kwa kawaida huonya juu ya kuunga mkono Iran yenye Washia wengi.
Makundi kadhaa kama yenye mismamo mikali yamewataka Waislamu wa Sunni kwa kauli moja kutojihusisha na upande wowote.
Pia shirika hilo huenda limechukua mkakati wa kuepuka kutoa matamshi zaidi dhidi ya Marekani au Israeli, kama lilivyofanya Februari 4.
Kwa sababu kufanya hivyo kunaweza kuonekana kama kuiunga mkono Iran kwa njia isiyo ya moja kwa moja, jambo ambalo linaweza kuharibu sifa yake miongoni mwa wafuasi wake.
Kwa upande wa itikadi, Washia wa Iran wanachukuliwa kuwa maadui wa jadi wa Waislamu wa Sunni.
Al-Qaeda walikuwa kimya wakati wa vita vya siku 12 vya Marekani na Israel dhidi ya Iran Juni 2025.
BBC





