Himid Mao yupo sana Azam FC.
Joyce Shedrack
June 19, 2026
Share :
Azam FC imemuongeza mkataba wa mwaka mmoja kiungo wake mkabaji Himid Mao ambaye zao la klabu hiyo ya Mitaa ya Chamazi.

Himid aliyerejea Azam FC mwanzoni mwa msimu huu akitokea nchini Misri alipokuwa anakipiga soka la kulipwa amefanya vyema na kuushawishi uongozi wa timu hiyo na kumpa mkataba mpya.
Katika ukurasa rasmi wa timu hiyo wametoa taarifa inayoonesha Azam FC imemuongezea mkataba Himid aliyewahi kuwa nahodha wa timu hiyo.





