Hizi hapa timu 10 muhimu kwenye magoli 900 ya Ronaldo
Sisti Herman
September 6, 2024
Share :

Baada ya jana kufanikiwa kufikisha mabao 900 kwenye maisha yake ya soka, hizi ni timu 10 ambazo Cristiano Ronaldo amezitumia kuandika rekodi muhimu;
▫️Goli la kwanza ni 7/10/2002 dhidi ya Moreirense
▫️Goli la 100 ni 27/01/2008 dhidi ya Spurs
▫️Goli la 200 ni 4/12/2010 dhidi ya Valencia
▫️Goli la 300 ni 5/5/2012 dhidi ya Granada
▫️Goli la 400 ni 6/1/2014 dhidi ya Celta Vigo
▫️Goli la 500 ni 30/9/2015 dhidi ya Molmo
▫️Goli la 600 ni 3/6/2017 dhidi ya Juventus
▫️Goli la 700 ni 14/10/2019 dhidi ya Ukraine
▫️Goli la 800 2/12/2021 dhidi ya Arsenal
▫️Goli la 900 5/9/2024 dhidi ya Croatia
Ronaldo alifunga goli moja lilimsaidia kufikia idadi hiyo kwenye mchezo wa UEFA Nations League dhidi ya Croatia ambapo Ureno wameshinda 2-1.
Goli lingine la Ureno kwenye mchezo huo lilifungwa na beki wa Manchester United huku pia akijifunga na kusaidia Croatia kupata goli la kufutia machozi.





