Hizi hapa timu 2 ambazo Henry kazipa ubingwa wa Champions League
Eric Buyanza
March 11, 2026
Share :
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry amezitaja Arsenal na Bayern Munich kama timu anazoona zinaweza kushinda UEFA Champions League msimu huu, akiwaacha nyuma Barcelona.
Henry amesema Bayern ni timu bora kuliko Barcelona, hivyo amewapa wajerumani hao nafasi ya ubingwa pamoja na Arsenal.
"Bayern Munich imekamilika zaidi kuliko Barcelona kwa jinsi wanavyoshambulia na kuhama nafasi,” Henry amesema.






