pmbet

Hormuz haitafunguliwa hadi trump atakapo ondolewa madarakani - Zolghadr

Eric Buyanza

September 18, 2026
Share :

Mohammad Baqer Zolghadr, mshauri wa kisiasa wa Mojtaba Khamenei, kiongozi mpya wa Jamhuri ya Kiislamu, amesema kuwa nchi yake haina nia ya kufungua Mlango-bahari wa Hormuz mradi tu Donald Trump aendelee kuwa madarakani.

 

Katika taarifa iliyochapishwa na mashirika ya habari nchini Iran siku ya Alhamisi, Bw. Zolqadr alisema: “Taifa hili limeazimia kuvunja pembe ya adui mchokozi na kuvunja migongo ya wenye kiburi.”
 

Aliendelea kusema kuwa Mlango-bahari wa Hormuz hautafunguliwa hadi pale Donald Trump na Benjamin Netanyahu watakapong'olewa kutoka "kiti cha madaraka," na kwamba hii ni "hatua ya kwanza ya kulipiza kisasi kwa taifa la Iran."

 

Sambamba na kauli nyingi na wakati mwingine zinazokinzana za Donald Trump kuhusu vita au mazungumzo na Iran, kuna mgawanyiko mkubwa wa maoni ndani ya nchi hiyo kuhusu iwapo waendelee na makabiliano ya kijeshi au wafanye mazungumzo na Marekani.

 

Wakati kundi la maafisa wa ngazi ya juu wa kisiasa nchini humo, kama vile Massoud Pezhikian na Mohammad Bagher Qalibaf, likitaka Marekani irejee kwenye masharti ya Mkataba wa Maelewano wa Islamabad na kuliona hilo kama sharti la kusitisha vita, watu wenye msimamo mkali akiwemo makamanda wa Walinzi wa Mapinduzi wanazungumzia kuendeleza vita na kuuweka Mlango-bahari wa Hormuz ukiwa umefungwa kama suluhisho madhubuti zaidi la kukabiliana na Marekani na Israel.

 

Wakati huo huo, kupanda kwa kasi kwa mfumuko wa bei, vikwazo vya kiuchumi, na kuzingirwa kwa bandari za kusini mwa Iran kwa njia ya maji kumeifanya hali ya maisha ya kila siku kwa raia wa nchi hiyo kuwa ngumu zaidi, huku kushuka kwa thamani ya sarafu ya Rial dhidi ya sarafu za kimataifa kukiongeza shinikizo zaidi kwenye hali ya maisha ya kila siku.

 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet