Hotuba ya mtoto Mtanzania iliyowakosha Viongozi wa dunia
Sisti Herman
November 19, 2024
Share :
Akihutubia sehemu ya Mkutano wa 29 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (COP-29) unaofanyika katika Mji wa Baku nchini Azerbaijan, mtoto Mtanzania Georgina Magesa ametoa wito kwa watu wote ulimwenguni kutunza mazingira ili kuepuka kutohatarisha maisha ya kizazi kijacho.
"Wapendwa viongozi wa dunia...kumbuka, unapolinda mazingira, unalinda afya ya watoto, elimu na ndoto zao. Na mtoto mwenye afya njema na aliyesoma anaweza kubadilisha ulimwengu!"
Hiyo ni sehemu ya nukuu za @georginamagesa akihutubia sehemu ya mkutano wa Watoto na vijana wa umoja wa mataifa kando ya Mkutano wa COP-29 ambao utafikia kilele chake tarehe 22 Novemba.