Ilibaki kidogo tu arudi nyumbani..! Miquissone atua Libya.
Joyce Shedrack
January 23, 2026
Share :
Klabu ya Al Ahly Benghazi ya Libya imenasa saini ya nyota wa zamani wa Simba na Al Ahly aliyekuwa akikipiga nyumbani kwao UD Songo Luis Miquissone akitokea klabu ya UD Songo.

Miquissone, ambaye amemaliza msimu huu nchini Msumbiji akiwa na tuzo ya Mchezaji Bora na Mfungaji Bora wa ligi ametambulishwa rasmi kuwa mchezaji wa klabu hiyo.





