Inter Miami yadhamiria kumsajili Casemiro
Sisti Herman
May 3, 2026
Share :

Inter Miami, wanashinikiza dili la kumsaini kiungo wa Brazil, Casemiro ambaye ameaga Manchester United na kuondoka mwisho wa msimu huu.
Mbrazil huyo amepanga kuondoka Man United tangu Januari huku akiwa tayari kwa sura mpya ya kibarua kuanzia msimu huu wa joto.
Inter Miami wako tayari kufanya hivyo kama ilivyofichuliwa mwezi Machi wakati mpango huo ukiendelea kuratibiwa.





