pmbet

Iran ni nchi yenye kiburi - Trump

Eric Buyanza

June 6, 2026
Share :

Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema Iran bado haijakubali makubaliano yaliyopendekezwa na Washington kwa sababu ni nchi yenye “nguvu” na “kiburi” na ndiyo maana sio rahisi kwao kukubali matakwa ya Marekani.

 

Trump alisema hayo akijibu maswali ya wanahabari.

Aidha kiongozi huyo aliongezea kuwa Iran imebakisha takriban 22% ya akiba yake ya makombora, na Marekani inaufahamu wa maeneo yaliyoko makombora hayo yaliyosalia pamoja na ndege zisizo na rubani.

 

Rais huyo wa Marekani alisema vituo vingi vya kutengeneza makombora, na maeneo ya kurushia silaha nchini Iran vimeharibiwa, ingawa Iran bado ina idadi fulani ya makombora na ndege zisizo na rubani.

 

Trump alikiri kuwa kuafikia makubaliano na Iran imekuwa jambo gumu ila bado anamatumaini la hilo kutokea.

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet