pmbet

IRAN YATOA ONYO KALI: "Tutashambulia Marekani na washirika wake"

Eric Buyanza

September 1, 2026
Share :

Iran imeonya kwamba nchi au taasisi yoyote iliyosaidia kupanga, kuwezesha au kushiriki katika shambulio la Marekani dhidi ya Kisiwa cha Larak italazimika kubeba gharama na kuwajibika kwa madhara yatakayofuata.

 

Tehran imesema wahusika hao watakabiliwa pia na jibu kali kutokana na hatua zao.

Katika barua yake kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama, balozi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amelaani shambulio hilo na kuitaka Marekani kusitisha kile Tehran inachokiita ukiukaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa, pamoja na hatua zinazotishia usafiri wa meli katika Ghuba ya Uajemi na Mlango wa Bahari wa Hormuz.

 

Jeshi la Iran pia limeonya kwamba litajibu dhidi ya nchi yoyote ambayo eneo lake litatumiwa kuanzisha mashambulizi dhidi ya Iran.

 

BBC

pmbet
pmbet

Leagues standings

Tanzania Premier League
pmbet
pmbet